Wednesday, January 22, 2014

OFFICIAL: TFF YAZUIA USAJILI WA EMMANUEL OKWI YANGA


USAJILI WA OKWI YANGA WAZUIWA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limesimamisha usajili wa mshambuliaji Emmanuel Okwi kutoka Uganda katika timu ya Yanga wakati likisubiri ufafanuzi kutoka Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA).
Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF iliyokutana leo (Januari 22 mwaka huu) kupitia masuala mbalimbali, imesimamisha usajili huo baada ya kubaini kuwa Okwi aliruhusiwa kuichezea SC Villa ya Uganda kwa kibali maalumu kutoka FIFA.
Okwi ambaye aliingia mgogoro na klabu yake ya Etoile du Sahel ya Tunisia aliruhusiwa na FIFA kuchezea SC Villa kwa kibali maalumu (provisional permit) cha miezi sita ili kulinda kiwango chake wakati suala lake dhidi ya Etoile du Sahel likishughulikiwa na shirikisho hilo la kimataifa.
Katika FIFA kuna kesi tatu kuhusiana na suala la mchezaji huyo. Wakati Okwi ameishitaki klabu hiyo FIFA kwa kutomlipa mshahara, Etoile du Sahel imemshitaki mchezaji huyo kwa utoro. Nayo Simba imeishitaki Etoile du Sahel kwa kushindwa kuilipa ada ya mauzo ya mchezaji huyo ambayo ni dola za Marekani 300,000.
Hivyo, TFF imeiandikia FIFA kutaka kujua iwapo mchezaji huyo anaweza kucheza Ligi nchini Tanzania wakati Etoile du Sahel ikiwa imefungua kesi katika shirikisho hilo la kimataifa ikidai Okwi bado ni mchezaji wake.
MECHI ZA TANZANIA PRISONS YAZASOGEZWA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limesogeza mbele mechi za raundi ya 14 na 15 zinazoihusu timu ya Tanzania Prisons zilizokuwa zichezwe Januari 25 na 29 mwaka huu.
Awali Tanzania Prisons ilitakiwa kutafuta uwanja mwingine wa kuchezea mechi hizo dhidi ya Ruvu Shooting na JKT Ruvu kutokana na Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine kutokuwa tayari kwa Ligi Kuu ya Vodacom wikiendi hii.
Mechi hizo sasa zitachezwa kati ya Februari 6 na 8 mwaka huu kwenye uwanja huo huo wa Kumbukumbu ya Sokoine.
Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari na Mawasiliano
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

CHELSEA WAKUBALI OFA YA £37M KUTOKA MAN UNITED KWA AJILI YA MATA - KUFANYIWA VIPIMO LEO


Ofa ya Manchester United ambayo inaaminika kuwa kiasi cha £37m, imekubaliwa na klabu ya Chelsea kwa ajili ya usajili kiungo wa kihispania Juan Mata.

Kiungo mwenye miaka 25 atafanyiwa vipimo vya afya leo Alhamisi kabla ya kukamilisha usajili wake wa kujiunga na mabingwa hao wa EPL.

Mata anategemewa kusaini mkataba wa miaka minne na nusu wa kuwepo Old Trafford.

Mhispania huyo, ambaye alikuwa mchezaji bora wa Chelsea katika misimu miwili iliyopita, aliwaaga wachezaji wenzie jana Jumatano katika uwanja wa mazoezi wa Chelsea - Cobham.

United hata hivyo wameendelea kukaa kimya kuhusu uthibitisho wa dili hilo huku kocha wa klabu hiyo akikataa kujibu swali kumhusu Mata baada ya kipigo kutoka kwa Sunderland katika nusu fainali ya kombe la ligi.

Waandishi wa habari walikuwa wametaarifiwa kabla ya mkutano wa baada ya mechi kwamba Moyes atajibu maswali kuhusu mechi tu na baadae walipojaribu kumuuliza kuhusu Mata, kocha huyo mscotish alijibu: "Hatusemi kitu chochote kuhusu hilo jambo."

Ikiwa uhamisho huo utakamilika basi United watakuwa wamevunja rekodi ya ada ya usajili ya klabu hiyo - walilipa kiasi cha £30.75m kwa Spurs kwa ajili ya kumsaini  Dimitar Berbatov  September 2008.

BREAKING NEWS: Mbunge wa Chalinze (CCM) afariki dunia

Mbunge wa jimbo la Chalinze (CCM) Said Ramadhani Bwanamdogo amefariki dunia leo asubuhi katika Taasisi ya Mifupo ya MOI alipokuwa amelazwa baada ya kuugua kwa muda mrefu.

#HABARI Mbunge wa jimbo la Chalinze (CCM) Said Ramadhani Bwanamdogo amefariki dunia leo asubuhi katika Taasisi ya Mifupo ya MOI alipokuwa amelazwa baada ya kuugua kwa muda mrefu.                   Said Ramadhani Bwanamdogo

HAYA SASA MAJANGA KWA WANAJANGWANI ETI MMILIKI WA YANGA AIBUKA,ATAKA KWENDA KWA KIKWETE

 BABUYANGA001
ALIYEJITANGAZA kuwa mmiliki
wa klabu ya Yanga, Juma
Mwambelo, amesema yu tayari
kukabidhi nyaraka
zinazotafutwa na uongozi wa
klabu hiyo kwa Rais wa
Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete.
Makamu Mwenyekiti wa Yanga,
Clement Sanga, alitangaza
kwenye mkutano wa Yanga
kwamba Mwambelo anashikilia
hati za umiliki wa klabu ya
Yanga kimakosa na anatakiwa
kuzikabidhisha haraka
iwezekanavyo kabla ya
kuchukuliwa hatua.
Akizungumza jana jijini Dar es
Salaam, Mwombelo alisema
yupo tayari kumpa Rais Kikwete
naye aukabidhi uongozi wa
Yanga chini ya Yusuf Manji.
“Kweli hati hizo ninazo kwa
kuwa mimi ni mmiliki wa Klabu
ya Yanga, ila Rais Kikwete pekee
ndiye naweza kumkabidhi, hata
mwanaye Ridhwani nimewahi
kumueleza kuhusiana na hili,”
alisema.
“Mimi ndiye mmiliki wa Klabu ya
Yanga, nina hati miliki halali ya
klabu, hii hapa (anaonyesha),
nina hati miliki ya jengo la
Jangwani, pia ninayo ya jengo la
Mafia, lakini hiyo waliiba na
tayari nilisharipoti polisi.
“Kuhusu hati ya jengo la
Jangwani ipo benki na yenyewe
sijailipia kwa kuwa kuna deni,
deni hilo ni zile fedha
ziliyotumika kujenga Uwanja wa
Kaunda. Hivyo,
deni likilipwa benki itakubali
kutoa hati kisha kuirudisha
wizarani na kutolewa rasmi.
“Nashangaa Yanga wanapodai
wanatumia katiba mpya, hii siyo
halali, katiba halali ya Yanga ni
ile ya mwaka 1967 ambayo
nakala yake hii hapa
(anaonyesha),” alisema.
Alipoulizwa juu ya uhalali wa
wanachama wa sasa wa klabu
hiyo, alisema: “Wanachama
wengine wote ni feki, mpaka
unatokea mgawanyiko mwaka
1975, wanachama halali wa
Yanga walikuwa 400, kuanzia
hapo hakuna wanachama halali
tena, hata akaunti zinazotumika
siyo za klabu.
“Hapa nilipo nimekuja polisi
(Magomeni) ili kutoa taarifa ya
kujihami, nahofia kupigwa
kutokana na walichokisema
kwenye mkutano,” alisema.
Katika mkutano mkuu wa
Jumapili, uliofanyika kwenye
Ukumbi wa Karume, PTA
Sabasaba jijini Dar es Salaam,
uongozi wa Yanga ulimtaja
mzee Juma kuwa ndiye aliyeiiba
hati ya jengo la klabu hiyo tangu
Juni 24, 2009.
“Mimi nilipigwa na watu mwaka
1987 nikapoteza fahamu kwa
siku tano, tangu pale sijawahi
kwenda klabuni wala uwanjani
kuitazama Yanga, hata huyo
Mrisho Ngassa simjui, namuona
tu kwenye magazeti, kikubwa
ninachotaka ni utaratibu
ufuatwe ndani ya Klabu ya
Yanga,” alisisitiza huku
akitabasamu.

PICHA ZA RIHANA ZAWA GUMZO MTANDAONI< NI PICHA ALIZOPIGA AKIWA BRAZIL> CHECK SWAGA HZOO

Rihanna ame-share picha zake akiwa kwenye mapumziko huko Brazil ambazo zinasambaa sana hivi sasa kwenye mtandao.
Rihanna akiwa Brazil ametumia muda huo pia kupiga picha kwa ajili ya cover ya Vogue Magazine.
Hizi picha amezipiga akila good time kwenye yatch.
6
5
4
3
2
1

sikiliza ngoma zinazo kamata kwa sasa

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...